Mafundisho Kuhusu Mungu (Teolojia)
Kozi hii inajenga uelewa na msingi wa kumjua Mungu kupitia njia mbalimbali alizotumia Mungu ili kumsaidia Mwanadamu kupata njia ya kuhusiana na Mungu.
Matokeo ya kujifunza
- Kueleza mamlaka ya Maandiko Matakatifu katika imani na maisha.
- Kufafanua fundisho la Utatu Mtakatifu kwa msingi wa Biblia.
- Kutambua kazi ya Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu katika mpango wa wokovu.
- Kuweka msingi imara wa kiteolojia kwa kozi nyingine zote zinazofuata.
Vitabu na miongozo
- Biblia Takatifu
- Imani za Msingi
- Seventh-day Adventists Believe
Yaliyomo katika kozi
Hakuna kitabu ambacho kimepata kupendwa, kuchukiwa, kuhofiwa, kushutumiwa kama Biblia. Watu wamekufa kwa ajili ya Biblia. Wengine wameua kwa ajili yake. Imehamasisha matendo makubwa na ya maana ya mwanadamu, na imelaumiwa kwa matendo maovu ya wanadamu. Vita vimepiganwa kwa ajili ya Biblia, mapinduzi yamepangwa kwa kusoma kurasa zake ...
-
Dakika 30-40Somo la 01: Msingi wa Maandiko MatakatifuUtangulizi • Ufunuo wa Mungu • Ufunuo wa kiujumla
-
Dakika 40-50Somo la 02: Ufafanuzi wa Maandiko MatakatifuUandishi wa Biblia • Uvuvio wa Maandiko • Mchakato wa Uvuvio
-
Dakika 30-40Somo la 03: Maendeleo ya Maandiko MatakatifuUvuvio na Historia • Usahihi wa Maandiko • Mamlaka ya Maandiko Matakatifu
-
Dakika 30-40Somo la 04: Matumizi ya Maandiko MatakatifuYesu na Mamlaka ya Maandiko • Roho Mtakatifu na Mamlaka ya Biblia • Kiwango cha Mamlaka ya Maandiko Matakatifu
-
Dakika 10-15Somo la 05: Muhtasari wa Maandiko Matakatifu
Kuna Mungu mmoja: Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, umoja wa Nafsi tatu za milele. Mungu asiyeweza kufikwa na mauti, mwenye enzi zote, mwenye uwezo wote, mwenye kujua yote, juu ya yote, na aliyepo daima. Hana kikomo na anapita ufahamu wa kibinadamu, walakini akijulikana kupitia ufunuo wake mwenyewe.
-
Dakika 20-30Somo la 06: Msingi wa Utatu MtakatifuUtangulizi • Mungu Aweza Kujulikana • Kupata Ufahamu wa Mungu
-
Dakika 40-50Somo la 07: Maendeleo ya Utatu MtakatifuUshahidi wa Maandiko Matakatifu • Mungu wa Maandiko Matakatifu • Matendo ya Mungu
-
Dakika 50-60Somo la 08: Matumizi ya Utatu MtakatifuUteule wa Asili na Uhuru wa Mwanadamu • Utendaji katika Utatu Mtakatifu • Mahusiano katika Utatu Mtakatifu
-
Dakika 10-15Somo la 09: Muhtasari wa Utatu Mtakatifu
Mungu Baba wa milele ni Mwumbaji, Chimbuko, Mtegemezaji, na Mfalme wa viumbe vyote. Ni mwenye haki na mtakatifu, mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na upendo na kweli. Tabia na uwezo vilivyoonyeshwa ndani ya Mwana na Roho Mtakatifu pia ni ufunuo wa Baba.
-
Dakika 30-40Somo la 10: Msingi wa Mungu BabaUtangulizi • Maoni juu ya Baba • Mungu wa Rehema
-
Dakika 50-60Somo la 11: Maendeleo ya Mungu BabaM ungu wa Kimbilio • M ungu wa Uaminifu • Mungu Baba Katika Agano Jipya
-
Dakika 10-15Somo la 12: Muhtasari wa Mungu Baba
Mungu Mwana wa milele alifanyika mwili katika Yesu Kristo. Katika Yeye vitu vyote viliumbwa, tabia ya Mungu imefunuliwa katika Yeye, wokovu wa jamii yote ya mwanadamu unakamilishwa na ulimwengu unahukumiwa. Milele zote Mungu kweli, Alifanyika mwanadamu kweli, Yesu aliye Kristo.
-
Dakika 50-60Somo la 13: Mungu MwanaUtangulizi • Kufanyika Mwili – Utabiri na Utimilifu wake • Onyesho la Kiunabii la Wokovu
-
Dakika 50-60Somo la 14: Ufafanuzi wa Mungu MwanaWakati wa Huduma yake na Kifo • Kufufuka kwa Mwokozi • Asili mbili za Yesu Kristo
-
Dakika 50-60Somo la 15: Maendeleo ya Mungu MwanaYesu Kristo ni Mwanadamu kweli kweli. • Kiwango cha kujitambulisha kwake na asili ya Mwanadamu • Muungano wa Asili Mbili
-
Dakika 40-50Somo la 16: Matumizi ya Mungu MwanaKristo ni Muungano wa Asili mbili • K uunganisha Asili Mbili • Umuhimu wa Kuunganisha Uungu na Uanadamu
-
Dakika 50-60Somo la 17: Muunganiko wa Mungu MwanaVyeo vya Yesu Kristo • Kristo Nabii • Kristo Kuhani
-
Dakika 10-15Somo la 18: Muhtasari wa Mungu Mwana
Mungu Roho Mtakatifu wa milele alikuwa mtendani pamoja na Baba na Mwana katika Uumbaji, katika Yesu kufanyika mwili na katika ukombozi. Aliwavuvia waandishi wa Maandiko Matakatifu. Alijaza maisha ya Yesu Kristo na uwezo. Huwavuta na kuasadikisha wanadamu; na wale wanaoitikia huwafanya upya na kuwabadilisha akiwapatia maisha mapya.
-
Dakika 50-60Somo la 19: Roho MtakatifuUtangulizi • Roho Mtakatifu ni Nani? • Roho Mtakatifu Kwa Uhalisi ni Mungu
-
Dakika 40-50Somo la 20: Maendeleo ya Roho MtakatifuUtume wa Roho Mtakatifu • Asili ya Utume • Hujaa kwenye mioyo ya Waumini
-
Dakika 10-15Somo la 21: Muhtasari wa Roho Mtakatifu
Kinachohitajika Ili Kujiunga
Kozi hii inafaa kwa kila mtu. Huhitajiki kozi yoyote kabla ya kujiandikisha — karibu ujiunga moja kwa moja!